8 Februari 2026 - 22:30
Hashd al-Shaabi yaharibu Handaki na Maficho ya ISIS Mashariki mwa Salahuddin

Hashd Al-Shaabi ya Iraq imefanikiwa kugundua na kuharibu handaki na maficho ya ISIS Mashariki mwa Salahuddin kwa kushirikiana na jeshi la Iraq, ikiwa ni sehemu ya juhudi za kuzuia kurejea kwa makundi ya kigaidi katika eneo hilo.

Shirika la Habari la Kimataifa la Ahlul-Bayt (as) -ABNA- Vikosi vya Hashd Shaabi vya Iraq vimetangaza kugundua na kuharibu handaki na maficho kadhaa ya wanachama wa kundi la kigaidi la ISIS (Daesh) mashariki mwa mkoa wa Salahuddin.

Operesheni hiyo imefanyika katika mfumo wa oparesheni ya pamoja ya kiusalama kwa ushirikiano na vikosi vya jeshi la Iraq, kwa lengo la kusafisha maeneo yaliyochafuliwa na kuzuia kurejea kwa harakati za seli za kigaidi.

Tags

Your Comment

You are replying to: .
captcha